Kikundi cha dance kinachofahamika kwa jina la Muda Africa kimeonyesha uwezo mkubwa wa kisanaa kwa kuonesha uchezaji wa dansi unaojulikana kama "Frozen Dance" uliowavutia na kuwaacha watazamaji vinywa wazi!Wanakikundi hao walionesha ubunifu, umakini na ushirikiano wa hali ya juu kwa kufanya miondoko iliyokuwa ikisimama ghafla kama sanamu na kisha kuendelea kwa ustadi mkubwa. Umahiri huo uliwafanya watazamaji kufurahia burudani hiyo huku wakitoa makofi na shangwe za pongezi.Maonesho haya yameendelea kuthibitisha kuwa sanaa ya dansi ni jukwaa muhimu la kuonesha vipaji, ubunifu na uwezo wa wasanii wa Tanzania katika kutoa burudani yenye mvuto kwa jamii.
"Vipaji huzaliwa, lakini wasanii huandaliwa. Karibu TaSUBa kwa mwaka wa masomo 2026/2027 ujifunze, ubobe na ufanikiwe katika dunia ya sanaa na utamaduni."
Nasoro Mchunga, mwanafunzi wa kozi ya Music and Sound Production katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa), ameendelea kuonesha umahiri wake katika sanaa ya ushairi, kipaji ambacho anasema alianza kukiendeleza mwaka 2020 alipokuwa mwanafunzi wa kidato cha kwanza.Nasoro anabainisha kuwa mapenzi yake kwa ushairi yalianza tangu akiwa shuleni, ambapo alianza kutunga mashairi mbalimbali yaliyolenga kuelimisha, kuburudisha na kuhamasisha jamii kuhusu masuala tofauti ya kijamii.Amewahimiza vijana wenye vipaji mbalimbali kuviendeleza kwa kujituma, kujifunza na kutokata tamaa, akisisitiza kuwa vipaji vinaweza kuwa daraja la kufikia mafanikio makubwa endapo vitapewa nafasi ya kukuzwa.
Copyright ©2024 Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) . All rights reserved.